Back
Benki ya UBA sasa yaunganishwa GePG
Jul 9, 2020
Mkuu wa kitengo cha sekta ya umma wa benki hiyo, Dominick Timothy, alisema na kueleza kuwa kwa sasa watu wataweza kulipa kwa haraka malipo ya kodi na yasiyo ya kodi kupitia UBA.
Alisema benki hiyo imepata kibali cha kuwa moja kati ya benki nane nchini zinazofanya malipo ya kodi na yasiyo ya kodi kwenda kwa taasisi za serikali kupitia mfumo wa GePG.
Timothy alisema kuwa kuunganishwa kwa benki yake katika mfumo wa GePG ni moja wapo ya njia za taasisi hiyo ya fedha kuunga mkono juhudi za maendeleo zinazofanywa na serikali chini ya Rais John Magufuli.
“Kutokana na benki yetu kuunganishwa na mfumo wa GePG itaoanisha mfumo huu na njia zake za kidijitali za kibenki ambazo ni kupata huduma kwa njia ya simu, mtandao na zile za Leo Chatbot, USSD Magic Banking na Webcollect,” alisema.
Alisema lengo la kuunganisha na njia hizo za kibenki ni ili kuwawezesha Watanzania kufanya malipo ya serikali popote pale walipo pasipo kulazimishwa kwenda katika tawi la benki.
0Shares
0Comments
0Favorites
0Likes
Say something to impress...
Loading...
Comments
Hot

No content at this moment.

Relevant people
Dira Ya Scooper
7792 Followers
Darubini ya Ulimwengu
Related