Back
Mzigo wa kansa waendelea kulemea wengi duniani
Feb 8, 2024
MZIGO wa maradhi ya kansa uneandelea kuongezeka.
Haya ni kulingana na makadirio yaliyotolewa na Shirika la kimataifa linalohusika na utafiti wa maradhi ya kansa (IARC).
Aidha, Shirika la Afya Duniani limechapisha matokeo ya aua kutoka mataifa 115, inayoonyesha kwamba nchi nyingi hazipi matibabu ya kansa kipaumbele, kama sehemu ya huduma ya afya kwa wote (UHC).
Aua ya WHO kuhusu UHC na kansa inaonyesha kwamba ni asilimia 39 pekee ya mataifa yaliyoshiriki, ambayo yalihusisha tiba ya kansa kama mojawapo ya huduma zinazogharimiwa.
Aidha, ni asilimia 28 pekee ya nchi zilizoshiriki ziligharamia huduma zingine za matibabu ya kansa, kama vile huduma ya kukabiliana na makali ya dalili za maradhi haya.
Kulingana na makadirio ya IARC, katika mwaka wa 2022 kulikuwa na takriban visa milioni 20 vipya vya kansa na vifo milioni 9.7. Idadi ya wagonjwa ambao waliendelea kuishi kwa miaka mitano baada ya kugundulika kuugua maradhi haya, ilikuwa milioni 53.5. Takriban mmoja kati ya watu watano hukumbwa na kansa, na takriban mmoja kati ya wanaume tisa na mmoja kati ya wanawake 12, hufariki kutokana na ugonjwa huu.
Kulingana na makadirio haya mapya ya IARC, aina 10 za kansa ziliwakilisha theluthi mbili ya visa vipya na vifo mwaka wa 2022.
Kansa ya mapafu ndio aina ya kansa iliyoonekana kukithiri sana ulimwenguni, huku visa milioni 2.5 vipya vikiwakilisha asilimia 12.4 ya visa vyote vya maradhi haya, vipya vilivyonakiliwa.
4Shares
0Comments
12Favorites
4Likes
Say something to impress...
Loading...
Comments
Hot

No content at this moment.

Relevant people
TAIFA LEO
951 Followers
Jukwaa la habari la ubora wa juu la ndani, linatarajia kuwasili kwako!
Related