Back
Mastaa wanaokwenda Kombe la Dunia la Klabu kibosi
May 17, 2025
NEW YORK, MAREKANI: KIVUMBI cha michuano mipya ya Fifa ya Kombe la Dunia la Klabu kinatarajiwa kuanza Juni 15 hadi Julai 13 na timu 32 zilizopangwa kwenye makundi manane ya timu nne, zitachuana kusaka ubingwa huo huko Marekani.
Miamba ya soka ya Ulaya kama Bayern Munich, Real Madrid na Manchester City ni miongoni mwa timu zitakazochuana kwenye michuano hiyo, ambayo itashuhudia mastaa kibao wanaolipwa mishahara mikubwa kwenye klabu zao wakionyeshana ubabe.
Wakati mashindano hayo ya Fifa yakiwa yamebakiza wiki chache kabla ya kuanza, hii hapa orodha ya wanasoka wanaoongoza kwa kulipwa mishahara mikubwa ambao watakwenda kuonyesha ubabe kuhakikisha timu wanazozitumikia zinaibuka na ushindi.
Kwa mujibu wa Capology, hii hapa orodha ya mastaa 11 wanaolipwa mishahara mikubwa ambao watakuwapo kwenye fainali hizo za Fifa kupigana vikumbo kuwania ubingwa.
11. Jan Oblak – Pauni 340,625 kwa wiki
Kipa huyo wa Atletico Madrid, Jan Oblak analipwa mkwanja wa maana kuliko makipa makini kabisa kama Ederson, Thibaut Courtois na Gianluigi Donnarumma, ambao wote watachuana kwenye michuano hiyo. Oblak ndiye kipa mwenye mshahara mkubwa zaidi wa wale watakaocheza fainali za Kombe la Dunia la Klabu. Mkataba wake utakwisha 2028 na analipwa Pauni 340,625 kwa wiki.
10. Vinicius Junior – Pauni 340,625 kwa wiki
12Shares
0Comments
14Favorites
6Likes
No content at this moment.